TANGAZO

Posted On: May 19, 2022


Habari Njema kwa Wateja Waliositishiwa Maji kwa Madeni

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Dodoma (DUWASA) inawakaribisha Wananchi waliositishiwa huduma ya maji kutokana na malimbikizo ya madeni kufika DUWASA ofisi Kuu chumba na. 31 kwa Afisa Mapato ili kusaini mikataba ya kurejeshewa huduma ya maji. Wateja husika watarejeshewa huduma ya maji kwa utaratibu ufuatao:

1.Kuingia mikataba ya kutakiwa kulipa madeni ya maji katika kipindi cha miezi mitatu hadi sita.

2.Mteja atatakiwa kulipa walau robo ya deni analodaiwa pamoja na ada ya kurejeshewa maji ya shilingi kumi na tano elfu (15,000/-).

3.Ulipaji wa madeni hayo utaenda sambamba na ulipaji wa bili ya maji ya kila mwezi bila kulaza baada ya kurejeshewa maji.

4.Utaratibu huu unawahusu wateja wa aina zote wa DUWASA wenye madeni ya maji kwa Jiji la Dodoma pamoja na miji ya Bahi, Kongwa na Chamwino.

5.Utaratibu wa unafuu huu unaanza tarehe 7/3/2022 hadi 16/09/2022.

Ndugu mteja wa DUWASA, kwanini ukae bila huduma ya maji wakati DUWASA imekurahisishia ulipaji wa deni lako? Tafadhali, tumia fursa hii muhimu na ya kipekee ili unufaike. Karibu sana kwenye Mamlaka yako ya DUWASA Makao Makuu ya Nchi - Dodoma.

Tangazo hili limetolewa na:

Eng. Aron Joseph

MKURUGENZI MTENDAJI

DUWASA